Select Menu

function googleTranslateEl

HABARI KIMATAIFA

HABARI KITAIFA

Performance

Cute

My Place

MICHEZO

Racing

Videos




Wakati picha za majengo yenye nyufa zikisambaa mitandaoni ikidaiwa ni ya hosteli mpya za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), uongozi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umekwenda kukagua ili kujiridhisha.

Majengo hayo yaliyojengwa na TBA kwa miezi minane yakielezwa kugharimu Sh10 bilioni yalizinduliwa Aprili 15,2017.

Ujenzi ulifanyika ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kumaliza tatizo la malazi kwa wanafunzi wa UDSM.

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa TBA, Elius Mwakalinga, jana alisema hata yeye ameziona picha hizo kwenye mitandao ya kijamii.

“Nimeziona na muda huu najiandaa kwenda huko kuangalia kama taarifa hizo ni za kweli,” al;isema Mwakalinga 

Picha hizo zilianza kusambaa jana jioni. Mwakalinga alisema huenda picha hizo ni za majengo mengine lakini zimehusishwa na hosteli hizo.

“Nitatoa taarifa baada ya kukagua majengo hayo kwa sasa siwezi kuzungumza hadi nitakapoona,” alisema.


Serikali imepanga kuajiri walimu 11,000 wa shule za msingi na sekondari katika mwaka wa fedha wa 2017/18.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Suleiman Jafo alisema katika mpango huo, walimu 7, 000 watakuwa wa shule za msingi na 4,000 wa sekondari.

“Hadi kufikia Desemba 31, walimu 2,700 watakuwa wameshaajiriwa,” alisema Jaffo

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma wakati wa kurekodi kipindi cha Tujadiliane kinachoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) na kurushwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari, Jafo alisema ajira hizo zitapunguza upungufu wa walimu unaotokana na ongezeko la wanafunzi tangu Sera ya Elimu Bure ya Msingi ianze kutekelezwa.

Tangu mwaka jana, Serikali inatekeleza sera hiyo inayoligharimu Taifa zaidi ya Sh20 bilioni kila mwezi, huku idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa katika shule za msingi na wale wanaojiunga na za sekondari ikiongezeka kwa zaidi ya wanafunzi milioni moja.

Kuhusu miundombinu shuleni alisema kwamba Serikali imetenga zaidi ya Sh37 bilioni za ujenzi wa mabweni katika shule za sekondari za umma 148.

Akifafanua, Jafo alisema zaidi ya Sh21 bilioni zimetumika kujenga mabweni 85 katika awamu ya kwanza ya mpango huo, huku awamu ya pili ya kujenga mabweni 65 iliyoanza kutekelezwa Agosti ikitarajiwa kugharimu Sh16 bilioni.

Kuhusu matundu ya vyoo na vyumba vya madarasa, Waziri Jafo alisema Serikali imetenga zaidi ya Sh246 bilioni kukabiliana na upungufu wa matundu ya vyoo na vyumba vya madarasa katika shule za umma.

“Theluthi moja ya fedha hizo, sawa na Sh82 bilioni zitatumika kukamilisha miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo inayotekelezwa kwa nguvu za wananchi,” alisema.

Waziri Jafo alisema kuwa Serikali imepanga kujenga vituo vya afya 172 kwa fedha kutoka Benki ya Dunia (WB), Serikali ya Canada na wadau wengine kupitia mfuko wa pamoja wa kuendeleza Sekta ya Afya (Basket Fund).

“Lengo ni kutekeleza sera ya zahanati kila kijiji na kituo cha afya katika kila kata ili kuwahakikishia wananchi upatikanaji wa huduma za afya,” alisema Jafo.

Alifafanua kuwa hivi sasa ni kata 530 pekee kati ya 3,900 zilizopo nchini ndizo zenye vituo vya afya.

Kuhusu upatikanaji wa dawa na vifaatiba, alisema Serikali imeongeza bajeti hadi kufikia Sh269 bilioni kwa ajili hiyo.

“Tunazo pia zaidi ya Sh127 bilioni za Basket Fund zitakazoelekezwa kwenye utatuzi wa changamoto ya upungufu wa dawa na vifaa tiba kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali za umma,” alisema.

Akizungumzia upungufu wa watumishi katika sekta ya afya iliyochangiwa na uhakiki wa vyeti feki, Waziri Jafo alisema tayari Serikali imeajiri watumishi 2,058 huku wengine zaidi wakitarajiwa kuajiriwa.

Suala la uhakiki wa vyeti lililoendeshwa na Serikali mwaka jana liliwanasa zaidi ya watumishi 19, 000 ambao ajira zao zilisitishwa, huku sekta ya afya na elimu zikiathirika Zaidi.






Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamis Kigwangalla, amefanya ziara ya kushtukiza katika bandari ya Dar es Salaam ambapo alibaini uwepo wa makontena yenye magogo ambayo ni mazao ya misitu yaliyokaa bandarini hapo kwa zaidi ya miaka 10.

Waziri Kigwangalla ameagiza Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii atangaze kujitokeza kwa wamiliki wa magogo hayo 938  na kama wamiliki wasipojitokeza, magogo hayo yatakuwa mali ya Serikali.

Aidha Dkt. Kigwangalla ametoa siku 30 kwa wamiliki wa makontena 55 yanayodaiwa kuingizwa nchini kutoka nchini Zambia kujitokeza na kuwasilisha nyaraka zao zenye kuthibitisha kama kweli yalivunwa nchini Zambia na yalivunwa wapi na kwa vibali gani vya nchi hiyo pamoja na kufuatilia nyaraka za kuingiza ndani ya Tanzania.

Ameagiza kitengo cha kuzuia ujangili kifuatilie kubaini uhalisia na uhalali wa taarifa hizo vinginevyo yatakuwa mali ya Serikali.

Dkt. Kigwangalla amefanya ziara ya kushtukiza bandarini hapo kufuatia uwepo wa taarifa za uvunaji holela wa magogo nchini, ambapo kuna taarifa kuwa kuna wafanyabiashara wa kigeni wanagawa vifaa vya kuvunia bure kwa ahadi ya kuuziwa mzigo na wahusika, pia uwepo wa taarifa kwamba kuna baadhi ya watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wanaotoa vibali na kugonga nembo kinyume cha taratibu za kisheria, hali inayotishia usalama wa raslimali adimu ya misitu yetu ya asili.






 



Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu wakifuatilia majadiliano na kuchangia hoja kuhusu Muswada wa Sheria ya Wakala wa Meli wa Taifa  baada ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani) kuwasilisha Muswada huo kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni mjini Dodoma.
..............................................................................................

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imedhamiria kuanzisha chombo cha kuendesha na kudhibiti sekta ndogo ya usafiri majini, usalama wa meli na mazingira ya bahari ili kulinda maslahi mapana ya taifa.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa wakati akijibu hoja ya Serikali kuhusu Muswada wa Sheria ya Wakala wa Meli wa Taifa mbele ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni mjini Dodoma.

Prof. Mbarawa amesema kuwa Serikali ipo kwenye mchakato wa kupeleka Muswada Bungeni wa kutunga sheria ambayo itaanzisha Shirika  la Wakala wa Meli wa Taifa (NASAC)  ambao utasimamia usalama wa meli na bahari zetu kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa bandari zetu kama mnavyojua bandarini kumekuwa na changamoto nyingi.

“Hivi karibuni tumeshuhudia upotevu wa mali na vitu vingi pale bandarini kama vile madini na vitu vingine vinaingia bila utaratibu,” amefafanua Prof. Mbarawa.

Ameongeza kuwa Serikali imeona ibadilishe mtazamo uliokuwepo zamani kupitia SUMATRA ambayo inasimamia masuala ya nchi kavu na majini, “Serikali imeona ianzishe chombo kingine ili kiweze kujikita kusamimia masuala ya usafiri wa majini pekee na masuala nyeti hasa ya uchumi wetu kama vile madini”.

Chombo kimoja cha kutoa huduma na kudhibiti sio jambo geni. Hapa nchini tunayo taasisi ya Mamlaka ya Anga Tanzania (TCAA) ambayo inatoa huduma ya anga na kudhibiti anga, hivyo Serikali inataka kufanya hivyo pia kwenye sekta ya usafiri wa majini.

Hili si jambo geni kwa kuwa linafanyika kwenye nchi nyingine kama vile ya bandari ya Singapore na nchi nyingine ya India.

Aidha, Prof. Mbarawa ametoa wito kwa wadau kushirikiana na Serikali kuanzisha chombo hiki. Pia amefafanua kuwa SUMATRA haitapokonywa majukumu yake bali nia ya Serikali ni kuitaka SUMATRA isimamie sekta ya nchi kavu tu kwa maana ya barabara, reli, magari ambayo ni sehemu kubwa na ina changamoto ambayo inahitajika kutatuliwa hivyo ijikite huko na sekta hii ndogo ya usafiri wa majini iwe na chombo kingine tofauti ili sheria iweze kutusaidia kukuza uchumi wa baharini na wa nchi kavu.

Ni imani ya Serikali kuwa, kwa kuwa na chombo cha udhabiti cha sekta ya nchi kavu ambapo NASAC itaanzishwa kwa ajili ya sekta ya usafiri wa majini, utaziwezesha sekta hizi za majini na nchi kavu kukua vizuri hivyo kukuza uchumi wetu, watanzania watapata ajira na kampuni nyingi za meli zitaingia nchini na kufanya kazi kwa kuwa mahali ambapo hakuna udhibiti sekta haiwezi kukua, “angalieni sekta nyingine kama ya mawasiliano ambako kuna udhibiti mzuri na sekta inakua vizuri” amesema Prof. Mbarawa.

Kwa mantiki hiyo, Serikali itawasilisha sheria ya SUMATRA Bungeni ili kufanyiwa maboresho ili iweze kuchangia vizuri ukuaji wa sekta ya nchi kavu na iende na wakati.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Prof.

Norman Sigalla King amesema kuwa azma ya Serikali ni nzuri katika muendelezo wa kuhakikisha kuwa taasisi zinazoanzishwa zina mgusa mlaji na kwa manufaa ya Serikali kwa ujumla. Serikali imejibu hoja zote za wadau na Kamati yetu inaendelea kuchambua hoja hizo ili kuhakikisha kuwa  inasimamia na kuishauri Serikali kwenye Muswada huu.

Ni dhamira ya Kamati kuona kuwa biashara bandarini inaendelea kuimarishwa na kudhibitiwa; na nchi yetu sio pekee yenye bandari kwenye ukanda huu hivyo ni lengo la Kamati kuhakikisha kuwa Muswada huu unaopendekezwa unaboreshwa ili kuhakikisha una akisi ushindani.

Ameongeza kuwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameelekeza udhibiti kwenye bandari yetu, hivyo huu ni mlolongo wa kusimamia na kudhibiti shughuli za uendeshaji wa bandari.

Kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe amewaomba Watanzania kukichangia Chama hicho ili kiweze kuwafikia na kuwaeleza mambo makuu mawili wakati wa mikutano ya kampeni ya udiwani.

ACT- Wazalendo imesimamisha wagombea 28 kati ya 43 katika uchaguzi mdogo wa udiwani utakaofanyika Novemba 26 ambapo kampeni zake zimeanza Oktoba 29.

“Nachukua fursa hii kuwaomba Watanzania wenye uchungu na nchi yetu kuchangia kampeni zetu. Tunataka kufika kila ya kona ya nchi yetu na wewe ndio utatuwezesha kufika,” amesema Zitto

“Chochote ulicho nacho tunaomba utuchangie kwa kutumia namba hizi hapa. Tigo pesa 0713957977 na M-Pesa 0744959112,  Asante Sana,” ameongeza

Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini Chama hicho kitatumia kampeni hizo kuwaeleza  Watanzania mambo makuu mawili ambayo ameyataja kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za wananchi na hali ngumu ya maisha ya wananchi.

“Lengo kubwa ni kuwaamsha Watanzania kukataa ubinywaji wa haki za binaadamu na kutaka mabadiliko ya sera za uchumi ili kuongeza ajira na kuondoa umasikini,” amesema Zitto

Amesema watatumia mifano halisi kwenye kata husika na kutoa sera mbadala kwa misingi ya Azimio la Tabora.

Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amembeza aliyekuwa mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu kwa kujivua uanachama wa chama hicho na kuonyesha dhamira ya kujiunga na Chadema.
 
Nape aliyewahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amekuwa mbunge wa pili wa CCM kuzungumzia uamuzi wa Nyalandu akitanguliwa na mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde ‘Kibajaji.’
 
Kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Twitter, Nape ameandika ujumbe ukiambatana na picha inayowaonyesha yeye, Nyalandu na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakiwa na nyuso za tabasamu.
 
Ujumbe huo ulisomeka “Chama cha siasa ni itikadi, itikadi ni imani, siamini sana katika kubadili imani kienyeji. Nitashughulikia mapungufu nikiwa ndani sio nje!”

Nape Moses Nnauye @Nnauye_Nape
Chama cha siasa ni ITIKADI, itikadi ni IMANI.Siamini SANA katika kubadili Imani KIENYEJI.Nitashughulikia MAPUNGUFU nikiwa ndani sio NJE!

HABARI KITAIFA




Wakati picha za majengo yenye nyufa zikisambaa mitandaoni ikidaiwa ni ya hosteli mpya za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), uongozi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umekwenda kukagua ili kujiridhisha.

Majengo hayo yaliyojengwa na TBA kwa miezi minane yakielezwa kugharimu Sh10 bilioni yalizinduliwa Aprili 15,2017.

Ujenzi ulifanyika ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kumaliza tatizo la malazi kwa wanafunzi wa UDSM.

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa TBA, Elius Mwakalinga, jana alisema hata yeye ameziona picha hizo kwenye mitandao ya kijamii.

“Nimeziona na muda huu najiandaa kwenda huko kuangalia kama taarifa hizo ni za kweli,” al;isema Mwakalinga 

Picha hizo zilianza kusambaa jana jioni. Mwakalinga alisema huenda picha hizo ni za majengo mengine lakini zimehusishwa na hosteli hizo.

“Nitatoa taarifa baada ya kukagua majengo hayo kwa sasa siwezi kuzungumza hadi nitakapoona,” alisema.


Serikali imepanga kuajiri walimu 11,000 wa shule za msingi na sekondari katika mwaka wa fedha wa 2017/18.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Suleiman Jafo alisema katika mpango huo, walimu 7, 000 watakuwa wa shule za msingi na 4,000 wa sekondari.

“Hadi kufikia Desemba 31, walimu 2,700 watakuwa wameshaajiriwa,” alisema Jaffo

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma wakati wa kurekodi kipindi cha Tujadiliane kinachoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) na kurushwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari, Jafo alisema ajira hizo zitapunguza upungufu wa walimu unaotokana na ongezeko la wanafunzi tangu Sera ya Elimu Bure ya Msingi ianze kutekelezwa.

Tangu mwaka jana, Serikali inatekeleza sera hiyo inayoligharimu Taifa zaidi ya Sh20 bilioni kila mwezi, huku idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa katika shule za msingi na wale wanaojiunga na za sekondari ikiongezeka kwa zaidi ya wanafunzi milioni moja.

Kuhusu miundombinu shuleni alisema kwamba Serikali imetenga zaidi ya Sh37 bilioni za ujenzi wa mabweni katika shule za sekondari za umma 148.

Akifafanua, Jafo alisema zaidi ya Sh21 bilioni zimetumika kujenga mabweni 85 katika awamu ya kwanza ya mpango huo, huku awamu ya pili ya kujenga mabweni 65 iliyoanza kutekelezwa Agosti ikitarajiwa kugharimu Sh16 bilioni.

Kuhusu matundu ya vyoo na vyumba vya madarasa, Waziri Jafo alisema Serikali imetenga zaidi ya Sh246 bilioni kukabiliana na upungufu wa matundu ya vyoo na vyumba vya madarasa katika shule za umma.

“Theluthi moja ya fedha hizo, sawa na Sh82 bilioni zitatumika kukamilisha miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo inayotekelezwa kwa nguvu za wananchi,” alisema.

Waziri Jafo alisema kuwa Serikali imepanga kujenga vituo vya afya 172 kwa fedha kutoka Benki ya Dunia (WB), Serikali ya Canada na wadau wengine kupitia mfuko wa pamoja wa kuendeleza Sekta ya Afya (Basket Fund).

“Lengo ni kutekeleza sera ya zahanati kila kijiji na kituo cha afya katika kila kata ili kuwahakikishia wananchi upatikanaji wa huduma za afya,” alisema Jafo.

Alifafanua kuwa hivi sasa ni kata 530 pekee kati ya 3,900 zilizopo nchini ndizo zenye vituo vya afya.

Kuhusu upatikanaji wa dawa na vifaatiba, alisema Serikali imeongeza bajeti hadi kufikia Sh269 bilioni kwa ajili hiyo.

“Tunazo pia zaidi ya Sh127 bilioni za Basket Fund zitakazoelekezwa kwenye utatuzi wa changamoto ya upungufu wa dawa na vifaa tiba kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali za umma,” alisema.

Akizungumzia upungufu wa watumishi katika sekta ya afya iliyochangiwa na uhakiki wa vyeti feki, Waziri Jafo alisema tayari Serikali imeajiri watumishi 2,058 huku wengine zaidi wakitarajiwa kuajiriwa.

Suala la uhakiki wa vyeti lililoendeshwa na Serikali mwaka jana liliwanasa zaidi ya watumishi 19, 000 ambao ajira zao zilisitishwa, huku sekta ya afya na elimu zikiathirika Zaidi.






Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamis Kigwangalla, amefanya ziara ya kushtukiza katika bandari ya Dar es Salaam ambapo alibaini uwepo wa makontena yenye magogo ambayo ni mazao ya misitu yaliyokaa bandarini hapo kwa zaidi ya miaka 10.

Waziri Kigwangalla ameagiza Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii atangaze kujitokeza kwa wamiliki wa magogo hayo 938  na kama wamiliki wasipojitokeza, magogo hayo yatakuwa mali ya Serikali.

Aidha Dkt. Kigwangalla ametoa siku 30 kwa wamiliki wa makontena 55 yanayodaiwa kuingizwa nchini kutoka nchini Zambia kujitokeza na kuwasilisha nyaraka zao zenye kuthibitisha kama kweli yalivunwa nchini Zambia na yalivunwa wapi na kwa vibali gani vya nchi hiyo pamoja na kufuatilia nyaraka za kuingiza ndani ya Tanzania.

Ameagiza kitengo cha kuzuia ujangili kifuatilie kubaini uhalisia na uhalali wa taarifa hizo vinginevyo yatakuwa mali ya Serikali.

Dkt. Kigwangalla amefanya ziara ya kushtukiza bandarini hapo kufuatia uwepo wa taarifa za uvunaji holela wa magogo nchini, ambapo kuna taarifa kuwa kuna wafanyabiashara wa kigeni wanagawa vifaa vya kuvunia bure kwa ahadi ya kuuziwa mzigo na wahusika, pia uwepo wa taarifa kwamba kuna baadhi ya watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wanaotoa vibali na kugonga nembo kinyume cha taratibu za kisheria, hali inayotishia usalama wa raslimali adimu ya misitu yetu ya asili.






 



Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu wakifuatilia majadiliano na kuchangia hoja kuhusu Muswada wa Sheria ya Wakala wa Meli wa Taifa  baada ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani) kuwasilisha Muswada huo kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni mjini Dodoma.
..............................................................................................

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imedhamiria kuanzisha chombo cha kuendesha na kudhibiti sekta ndogo ya usafiri majini, usalama wa meli na mazingira ya bahari ili kulinda maslahi mapana ya taifa.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa wakati akijibu hoja ya Serikali kuhusu Muswada wa Sheria ya Wakala wa Meli wa Taifa mbele ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni mjini Dodoma.

Prof. Mbarawa amesema kuwa Serikali ipo kwenye mchakato wa kupeleka Muswada Bungeni wa kutunga sheria ambayo itaanzisha Shirika  la Wakala wa Meli wa Taifa (NASAC)  ambao utasimamia usalama wa meli na bahari zetu kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa bandari zetu kama mnavyojua bandarini kumekuwa na changamoto nyingi.

“Hivi karibuni tumeshuhudia upotevu wa mali na vitu vingi pale bandarini kama vile madini na vitu vingine vinaingia bila utaratibu,” amefafanua Prof. Mbarawa.

Ameongeza kuwa Serikali imeona ibadilishe mtazamo uliokuwepo zamani kupitia SUMATRA ambayo inasimamia masuala ya nchi kavu na majini, “Serikali imeona ianzishe chombo kingine ili kiweze kujikita kusamimia masuala ya usafiri wa majini pekee na masuala nyeti hasa ya uchumi wetu kama vile madini”.

Chombo kimoja cha kutoa huduma na kudhibiti sio jambo geni. Hapa nchini tunayo taasisi ya Mamlaka ya Anga Tanzania (TCAA) ambayo inatoa huduma ya anga na kudhibiti anga, hivyo Serikali inataka kufanya hivyo pia kwenye sekta ya usafiri wa majini.

Hili si jambo geni kwa kuwa linafanyika kwenye nchi nyingine kama vile ya bandari ya Singapore na nchi nyingine ya India.

Aidha, Prof. Mbarawa ametoa wito kwa wadau kushirikiana na Serikali kuanzisha chombo hiki. Pia amefafanua kuwa SUMATRA haitapokonywa majukumu yake bali nia ya Serikali ni kuitaka SUMATRA isimamie sekta ya nchi kavu tu kwa maana ya barabara, reli, magari ambayo ni sehemu kubwa na ina changamoto ambayo inahitajika kutatuliwa hivyo ijikite huko na sekta hii ndogo ya usafiri wa majini iwe na chombo kingine tofauti ili sheria iweze kutusaidia kukuza uchumi wa baharini na wa nchi kavu.

Ni imani ya Serikali kuwa, kwa kuwa na chombo cha udhabiti cha sekta ya nchi kavu ambapo NASAC itaanzishwa kwa ajili ya sekta ya usafiri wa majini, utaziwezesha sekta hizi za majini na nchi kavu kukua vizuri hivyo kukuza uchumi wetu, watanzania watapata ajira na kampuni nyingi za meli zitaingia nchini na kufanya kazi kwa kuwa mahali ambapo hakuna udhibiti sekta haiwezi kukua, “angalieni sekta nyingine kama ya mawasiliano ambako kuna udhibiti mzuri na sekta inakua vizuri” amesema Prof. Mbarawa.

Kwa mantiki hiyo, Serikali itawasilisha sheria ya SUMATRA Bungeni ili kufanyiwa maboresho ili iweze kuchangia vizuri ukuaji wa sekta ya nchi kavu na iende na wakati.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Prof.

Norman Sigalla King amesema kuwa azma ya Serikali ni nzuri katika muendelezo wa kuhakikisha kuwa taasisi zinazoanzishwa zina mgusa mlaji na kwa manufaa ya Serikali kwa ujumla. Serikali imejibu hoja zote za wadau na Kamati yetu inaendelea kuchambua hoja hizo ili kuhakikisha kuwa  inasimamia na kuishauri Serikali kwenye Muswada huu.

Ni dhamira ya Kamati kuona kuwa biashara bandarini inaendelea kuimarishwa na kudhibitiwa; na nchi yetu sio pekee yenye bandari kwenye ukanda huu hivyo ni lengo la Kamati kuhakikisha kuwa Muswada huu unaopendekezwa unaboreshwa ili kuhakikisha una akisi ushindani.

Ameongeza kuwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameelekeza udhibiti kwenye bandari yetu, hivyo huu ni mlolongo wa kusimamia na kudhibiti shughuli za uendeshaji wa bandari.

Kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe amewaomba Watanzania kukichangia Chama hicho ili kiweze kuwafikia na kuwaeleza mambo makuu mawili wakati wa mikutano ya kampeni ya udiwani.

ACT- Wazalendo imesimamisha wagombea 28 kati ya 43 katika uchaguzi mdogo wa udiwani utakaofanyika Novemba 26 ambapo kampeni zake zimeanza Oktoba 29.

“Nachukua fursa hii kuwaomba Watanzania wenye uchungu na nchi yetu kuchangia kampeni zetu. Tunataka kufika kila ya kona ya nchi yetu na wewe ndio utatuwezesha kufika,” amesema Zitto

“Chochote ulicho nacho tunaomba utuchangie kwa kutumia namba hizi hapa. Tigo pesa 0713957977 na M-Pesa 0744959112,  Asante Sana,” ameongeza

Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini Chama hicho kitatumia kampeni hizo kuwaeleza  Watanzania mambo makuu mawili ambayo ameyataja kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za wananchi na hali ngumu ya maisha ya wananchi.

“Lengo kubwa ni kuwaamsha Watanzania kukataa ubinywaji wa haki za binaadamu na kutaka mabadiliko ya sera za uchumi ili kuongeza ajira na kuondoa umasikini,” amesema Zitto

Amesema watatumia mifano halisi kwenye kata husika na kutoa sera mbadala kwa misingi ya Azimio la Tabora.

Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amembeza aliyekuwa mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu kwa kujivua uanachama wa chama hicho na kuonyesha dhamira ya kujiunga na Chadema.
 
Nape aliyewahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amekuwa mbunge wa pili wa CCM kuzungumzia uamuzi wa Nyalandu akitanguliwa na mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde ‘Kibajaji.’
 
Kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Twitter, Nape ameandika ujumbe ukiambatana na picha inayowaonyesha yeye, Nyalandu na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakiwa na nyuso za tabasamu.
 
Ujumbe huo ulisomeka “Chama cha siasa ni itikadi, itikadi ni imani, siamini sana katika kubadili imani kienyeji. Nitashughulikia mapungufu nikiwa ndani sio nje!”

Nape Moses Nnauye @Nnauye_Nape
Chama cha siasa ni ITIKADI, itikadi ni IMANI.Siamini SANA katika kubadili Imani KIENYEJI.Nitashughulikia MAPUNGUFU nikiwa ndani sio NJE!